Kwenye kikao cha Bunge leo April 13 Waziri wa nishati na Madini January Makamba amewakaribisha watu wenye uwezio wa kusaidia kuleta mafuta kwa bei nafuu kwenye ofisi yake ili waweze kusaidia nchi,baada ya baadhi ya wabunge kueleza kuwa kuna uwezekano wa mafuta ya bei rahisi kupatikana.
“Mtu yeyote, pahala popote, Mtanzania yeyote mwenye taarifa au uwezo wa kuisaidia nchi kuleta mafuta ya bei nafuu karibu sana ofisini hata leo ili tuzungumze, hatuwezi kung’ang’ania kitu kumbe kuna kitu kingine kitatusaidia zaidi, nchi hii ni yetu wote,” Ameeleza Waziri Makamba
#spinupdates